Matokeo ya kidato cha nne 2023/2024. Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA) leo January 25,2024 limetangaza matokeo ya mtihani wa kidato cha nne uliofanyika November 2023 ambapo jumla ya Watahiniwa 484,823 sawa na 87.65% ya Watahiniwa waliofanya mtihani huo wamefaulu.
![]() |
“Kati ya Wanafunzi hao waliofaulu kuna Watahiniwa wa Shule na Watahiniwa wa Kujitegemea ambapo jumla ya Watahiniwa wa Shule 471,427 kati ya 527,576 wenye matokeo ambao ni sawa na 89.36% wamefaulu ambapo wamepata madaraja ya I, II, III na IV, mwaka 2022 Watahiniwa waliofaulu walikuwa 456,975 sawa na 87.79% hivyo ufaulu
umeongezeka kwa 1.57%“
“Watahiniwa wa Kujitegemea waliofaulu mtihani ni 13,396 sawa na 52.44%, mwaka 2022 Watahiniwa wa kujitegemea 19,475 sawa na 68.34%!walifaulu mtihani huo. hivyo, faulu wa Watahiniwa hao wa kujitegemea umeshuka kwa 15.90% na mwaka 2022”
Social Plugin