Ad Code

Matokeo ya kidato cha nne 2023/2024.

Matokeo ya kidato cha nne 2023/2024. Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA) leo January 25,2024 limetangaza matokeo ya mtihani wa kidato cha nne uliofanyika November 2023 ambapo jumla ya Watahiniwa 484,823 sawa na 87.65% ya Watahiniwa waliofanya mtihani huo wamefaulu. 

Matokeo ya kidato cha nne 2023
Akitangaza matokeo hayo Jijini Dar es saaam, Katibu Mtendaji Baraza la Mitihani la Tanzania, Dkt. Said Ally Mohamed amesema “Wasichana waliofaulu ni 257,892 sawa na 86.17% wakati Wavulana waliofaulu ni 226,931 sawa na 89.40%, mwakaa 2022 Watahiniwa waliofaulu walikuwa ni 476,450 sawa na 86.78%, hivyo ufaulu wa Watahiniwa umeongezeka kwa 0.87% ikilinganishwa na mwaka 2022”


“Kati ya Wanafunzi hao waliofaulu kuna Watahiniwa wa Shule na Watahiniwa wa Kujitegemea ambapo jumla ya Watahiniwa wa Shule 471,427 kati ya 527,576 wenye matokeo ambao ni sawa na 89.36% wamefaulu ambapo wamepata madaraja ya I, II, III na IV, mwaka 2022 Watahiniwa waliofaulu walikuwa 456,975 sawa na 87.79% hivyo ufaulu
umeongezeka kwa 1.57%“

“Watahiniwa wa Kujitegemea waliofaulu mtihani ni 13,396 sawa na 52.44%, mwaka 2022 Watahiniwa wa kujitegemea 19,475 sawa na 68.34%!walifaulu mtihani huo. hivyo, faulu wa Watahiniwa hao wa kujitegemea umeshuka kwa 15.90% na mwaka 2022”

Matokeo ya kidato cha nne 2023/2024.

Reactions

Ad Code

Responsive Advertisement